Sunday, April 28, 2013

Anataka Awe Nyumba Ndogo Yangu:Nifanyeje?


Wapendwa habari za majukumu ya kulijenga taifa.

 Nikiwa katika pitapita zangu miezi mitatu iliyopita; nikikutana na mwanadada mrembo; nikawa nimekaa naye meza moja. Katika kuongea ongea akanipa historia ya maisha yake. Kikubwa ni kwamba aliolewa lakini tabia ya mume wake kumpa kichapo mara kwa mara aliamua kuomba uamisho kazini na kuhama toka kwenye mji anapoishi mume wake. 

Kwa kuwa tuliendelea kuwa na mawasiliano; siku moja akanikaribisha nyumbani kwake; nikakuta amejiandaa kisawasawa; mambo ya kikubwa yakaendelea, jioni nikatoka naye out; haikuishia hapo tukaendelea kama wapenzi. Majuzi ananambia eti anataka anizalie mtoto na anitambulishe hadi kwa ndugu zake. 


Nashindwa kumpa ok kwa kuwa mi tayari nina mke; na mume wake bado anambembeleza warudiane. Yeye anadai awezi kurudiana na huyo mwanaume kwa sababu ni mkorofi na anamdunda mara kwa mara; mtoto wa watu ana makovu hadi namuonea huruma. Naomba ushauri wako we unayesoma hii habari.
by 

No comments:

Post a Comment