Monday, April 29, 2013

"ATAKAYEKUBALI KUIVUNJA CHADEMA ATALAANIWA HAPA DUNIANI MPAKA MBINGUNI ".....ZITTO KABWE...!!

WAKATI Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, akisema kuwa chama chake sasa hakitawapokea na kuwapa nafasi za uongozi wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaofukuzwa, mkakati wa kukivuruga chama chake umebainika, MTANZANIA Jumapili linaripoti.

Mbowe, wakati akitoa kauli hiyo jana mkoani Tabora, taarifa zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa mkakati unaodaiwa kuandaliwa na chama dola kukidhoofisha Chadema unaendelea kuratibiwa kwa karibu na ‘virusi’ (mashushu) waliopenyezwa ndani ya chama hicho na huenda yakaibuliwa mambo mengi zaidi yanayodaiwa kufanywa na chama hicho.

Aidha matukio yanayotokea bungeni, nguvu za dola kutumika kupita kiasi, uwepo wa ‘virusi’ ndani ya chama hicho ni miongoni mwa mambo yanayotajwa na baadhi ya maofisa wa ngazi za juu wa vyombo vya ulinzi na usalama kwamba chama hicho kinaandaliwa anguko.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa mkakati wa kukidhoofisha Chadema ulianza tangu siku nyingi na unaratibiwa kwa ukaribu na ‘virusi’ wanaodaiwa kupenyezwa ndani ya chama hicho, ambacho katika siku za hivi karibuni kimepata uungwaji mkono mkubwa.

Inaelezwa kuwa kumekuwa na juhudi kubwa zinazofanywa na mahasimu wa Chadema kutaka kukidhoofisha chama hicho kupitia harakati zake za kisiasa, ambazo imekuwa ikizifanya kwenye mwanga na gizani.

No comments:

Post a Comment