Friday, April 5, 2013

MOVIE MPYA KUHUSU TAMU NA CHUNGU ZA KAJALA

Straight kutoka Bongomovie muigizaji maarufu nchini anae celebrate freedom yake uraiani kwasasa talk about Kajala amefunguka kuhusu mpango wake wa kushoot filamu itakayo yaanika maisha yake halisi kutoka kitaa hadi gerezani.
Kajala ambae hivi kaibuni aliponea chupuchupu
kuhukumiwa kifungo cha miaka 7 jela kutokana na tuhuma za kushirikiana na mume wake Faraji Augustino kutumia visivyo fedha za serikali amesema filamu hiyo ina lengo la kutoa elimu ya namna ya kujiepusha na mazingira yanayoweza kugharimu muda na maisha ya mtu.
Gonga continue reading kuendelea..

Hata hivyo kufuatia uvumi kuwa Star huyo alichora tattoo yenye jina la Wema Sepetu mgongoni kwake kama ishara ya kurudisha fadhila kwa shost yake amekanusha na kusema kuwa kwasasa ni mapema kusema kuwa anaweza kumlipa wema fadhila isipokuwa tattoo mgongoni kwake ni ishara ya appreciations kwa rafiki yake.
Muigizaji huyo ambae amemtaja Wema Sepetu kama Hero wake amewataka mabinti kutokimbilia mali za wanaume bila kujua zinavyopatikana na badala yake wajishughulishe ili kuepuka hatari ya kungia kwenye mkumbo utakao yagharimu maisha yao.
Huenda Jumamosi hii ikafanyika ‘Get together party’ Ambasador Launge maalumu kwa ajili ya Kajala ambapo kila mtu ataingia kwa kiingilio cha shilingi 10,000 lengo ikiwa ni kuwezesha watu mablimbali kukutana na msanii huyo asilimia 50% ya fedha zitakazo patikana ikiwa ni halali yake.

No comments:

Post a Comment