Wednesday, May 22, 2013

UWOYA, JOHARI KUZURU SAUZI....!!!

Irene Uwoya.
MASTAA wa sinema za Kibongo, Irene Uwoya na Blandina Chagula ‘Johari’ wametimkia nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’ kwenda kurekodi filamu. Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni kwa njia ya simu akiwa nchini humo, Uwoya alisema wamekwenda nchini humo kurekodi sinema ambayo Watanzania wataitambua ikikamilika. Pia wataunganisha na ziara ndefu katika nchi mbalimbali barani Afrika zikiwemo Namibia, Ghana, Lesotho na kwingineko kujifunza soko la filamu.
 
Blandina Chagula ‘Johari’.
“Tupo huku na Johari lakini tutakuwa na ziara ndefu sana ya nchi mbalimbali za Afrika kwa ajili ya kulisogeza soko letu la filamu na kujifunza jinsi wenzetu wanavyofanya katika filamu zao,” alisema Uwoya.

No comments:

Post a Comment