Tuesday, May 7, 2013

Chris Brown athibitisha hayupo tena na Rihanna

Chris Brown amethibitisha kuwa ameachana tena na mpenzi wake Rihanna

Juzi Jumapili muimbaji huyo wa ‘Fine China’ alisherehekea birthday yake ya kutimiza umri wa miaka 24 kwa kuangusha party za nguvu katika majiji ya Las Vegas, New York na Los Angeles, na kuweka wazi kuwa yupo single na anaweza kujirusha na wasichana wengi atakao licha ya kudai bado anampenda Rihanna wanayeachana na kurudiana kila mara.
Rihanna – ambaye alidai kuwa alipanga surprise ya nguvu kwa Breezy, hakuhudhuria party yoyote kati ya hizo kwakuwa alikuwa busy kuperform kwenye ziara yake ya ‘Diamonds World Tour’ weekend hii.

Credits:Bongo 5

No comments:

Post a Comment