Friday, May 10, 2013

MUME WA JACK PATRICK AIKANA NDOA YAKE BAADA YA KUTOKA JELA


\


Abdullatif Fundikira ‘Tiff” akiwa na mkewe Jacqueline Patrick kabla ya kwenda jela.
MUME wa mwanamitindo maarufu hapa Bongo, Jacqueline Patrick, Abdullatif Fundikira ‘Tiff”, aliyekuwa jela ya Gereza la Keko jijini Dar alikokuwa akishikiliwa kwa tuhuma za kufanya biashara ya madawa ya kulevya, amerudi uraiani baada ya kupata dhamana.


Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, Tiff aliachiwa kwa dhamana Ijumaa iliyopita katika Mahakama  ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kusota ‘lupango’ kwa takriban mwaka mmoja.

               

JACK PATRICK KATIKA POZI “Ni kweli sasa hivi Tiff yuko mtaani, ametoka kwa dhamana ila kuhusiana na suala la ndoa yake amesema haipo tena, anaangalia maisha yake,” kilidai chanzo.
Katika kupata ukweli wa habari hii, mwandishi wetu alimpigia simu Abdullatif lakini hakupokea ila Jack alipopatikana alikiri zilipendwa wake huyo kuachiwa kwa dhamana.

No comments:

Post a Comment