Sunday, May 12, 2013

MSICHANA WA MIAKA 16 APIGWA RISASI BAADA YA KUKUTWA ANASHIRIKI TENDO LA NDOA NDANI YA GARI NA MWANAUME JIJINI DAR


 


JESHI la polisi limekumbwa na
 kashfa nyingine baada ya askari wake
 kudaiwa kumpiga risasi msichana wa
 miaka 16 baada ya kumkuta akivunja amri ya sita ndani ya gari.
Msichana huyo..
(Jina tunalihifadhi) alikumbana na mkasa huo
 Jumatano usiku eneo la Mbagala Zakhem
 jijini Dar es Salaam, ambapo alipigwa
 risasi sehemu ya makalio wakati
 akijaribu kuwakimbia polisi kwa 

kutumia gari la mpenzi wake.
Mpenzi huyo (jina linahifadhiwa), 
alikamatwa na kuwekwa mahabusu na
 kufunguliwa kesi ya ubakaji.

Akizungumza na NIPASHE Jumapili jana katika wodi
 ya Hospitali ya Temeke alikolazwa, msichana
 huyo alisema siku ya tukio alikutana na
 kijana huyo majira ya saa 8:00 usiku
 katika baa moja inayoitwa Kindau na
 kukubaliana kwenda kushiriki 
tendo la ndoa kwa malipo ya Sh 20,000.
Alisema kutokana na muda huo kuwa
 usiku sana hawakuweza kwenda katika
 nyumba ya kulala wageni na badala yake
 walikwenda eneo la Zakhem na kisha
 walipaki gari kwenye uchochoro na
 baadae walianza kubanjua amri ya sita.
Wakiwa kwenye kilele cha mapenzi yao
, ghafla walishtukia gari la polisi likiwajia 
kwa kasi kwa nia ya kuwakamata.


“Tuliagana anilipe elfu ishirini wala
 hakunibaka kama anavyodai, wao 
polisi walitukuta tayari tunamaliza
 lakini kutokana na woga 
tulikimbia ili tusikamatwe,” alisema msichana huyo.

Alisema wakati wanakimbia 
kwa kutumia gari la mpenzi wake
 askari mmoja alifyatua risasi
 iliyopenya kwenye taa ya gari na
 kwenda kumjeruhi sehemu ya makalio yake.

“Nilisikia mlio mkubwa wa bunduki,
 ghafla nilihisi kitu kimeingia mwilini
 mwangu na kuishiwa nguvu,” alisema kwa uchungu.

Alisema kwa kuona hali hiyo, 
mpenzi wake alisimamisha gari kwa 
kujisalimisha na polisi walipowafikia
 walimtaka mpenzi wake huyo atoe pesa
 kama malipo ya kitendo chao cha 
kukutwa wakifanya mapenzi
 ama sivyo watampeleka kituoni.

Alieleza kuwa mpenzi wake hakuweza
 kutoa pesa hizo ndipo walipoamua
 kumpiga na kumpeleka kituo cha
 polisi cha Mbagala na yeye alifikishwa 
hospitalini hapo kwa ajili ya matibabu.

Hata hivyo, ndugu na jamaa wa mpenzi
 wake wanapinga hatua ya polisi hao
 kutumia nguvu kubwa kama watu hao
 walikuwa watuhumiwa wa ujambazi.

Wakizungumza wakiwa kwenye kituo 
cha Polisi cha Mbagala kufuatilia
 hatma ya ndugu yao, ndugu hao
 ambao hawakutaka majina yao 
yatajwe gazetini walisema hatua ya
 polisi kupiga risasi huku wakitambua
 watu hao sio majambazi ni kitendo cha kinyama.

“Tunachoshangaa ni kwa nini polisi
 wapige risasi wakati wakijua hawakuwa
 majambazi ila walikuwa wakifanya 
mapenzi, hata hilo jalada la kesi 
walilofungua wanataka kuficha maovu
 yao na sio vinginevyo,” alisema ndugu
 mmoja ambaye alijitambulisha kuwa shemeji yake.

Alisema kimsingi tukio hilo lilikwenda 
katika makubaliano yao na sio ubakaji
 kama wanavyodai, ila kinachofanyika
 kwa sasa ni kutaka kumlinda askari
 mwenzao aliyejeruhi kwa risasi.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Temeke,
 David Misime, alipopigiwa simu kuelezea 
tukio hilo, alisema kwa sasa hawezi
 kulizungumza kwa kuwa yupo nje ya Mkoa kikazi.
Dj Sek Blog

No comments:

Post a Comment