Tuesday, May 14, 2013

MDAU MKUBWA WA BONGO FLAVA AMCHANA MRISHO MPOTO.

blog1.jpg



Huyu Mpoto naanza kupata tafsiri tofauti kidogo juu yake na kuanza kuamini kwamba katumiwa kuangusha madai ya msingi sana, support ya muziki by CFM iz obvious n undisputed BUT it was supposed to be beyond obvious and non discriminatory, ye mwenyewe kazungumza kuhusu Tanzania na mambo ambayo hayaendi sawa katika tungo zake, haimanishi kwamba serikali haijafanya chochote. Kuna mambo ambayo hayaendi sahihi ndo maana kazungumzia katika nyimbo zake. Jay Dee kama alivyo Mpoto kwa maana kwamba wote ni wasanii na watunzi na zaidi maisha yao yamejikita katika muziki, kwa mlinganyo sawa kama ulivyoimba uhalisia juu ya Tanzania, Jay Dee pia kaamua kuyasema anayoona si sawa na kila mmoja anatambua. Alichokifanya Mpoto ni sawa na mtu mwingine yule aibuke leo na kusema kwamba Mpoto anamsema vibaya mjomba, lazima atawashanganza wote wenye busara. Hivyo ndivyo Mpoto alivyowashangaza Watanzania wenye busara na wapenda maendeleo ya muziki wa Kitanzania.

No comments:

Post a Comment