Thursday, May 9, 2013

MAKAMU MKUU WA CHUO CHA SAUT NAYE APINGA KUFUTWA KWA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

Katika kipindi cha Tuongee asbuhi Makamu mkuu wa chuo cha SAUT Father Charles Kitima amesema kitendo  cha  bunge kuingilia Baraza la mitihani na kutaka  mitihani isahihishe upya ni kuvunja sheria ya nchi. ....


Kitima  amesema wanaosema mitihani isahihishwe upya hawana vision ya nchi hii kwani wako Bungeni kupiga madawati na kufundisha watoto matusi kwa hiyo hawana weledi wa kuongoza nchi hii.
 
Makamu  huyo  ameongeza  kwa kusema Rais wanamlaum bure kwa sababu kuna waziri wa elimu MPUMBAVU ambaye  ndiye  anayepaswa  kulaumiwa


Amesema bunge letu linatumiwa vibaya na wabunge walio wengi kwa kupitisha kila kitu kinacho jali masilahi yao wakati wao watoto wao wako nje ya nchi,pia akaongezea kwa kusema nchi hii imekufa usalama hakuna elimu imekufa na watu wanatumia bunge vibaya. 

No comments:

Post a Comment